JavaScriptin tulee olla päällä. This page requires JavaScript. Den sida kräver JavaScript.
UCHUNGUZI WA WAZAZI 2018
KWA WAZAZI HADI WATOTO KATIKA ELIMU MSINGI (SHULE YA WATU WOTE)
Ushirikiano kati ya wazazi na shule ni muhimu kwa ustawi wa watoto na mafunzo ya mafanikio shuleni. Shirika la wazazi wa Kifini na Kiswidi (Suomen Vanhempainliitto na Förbundet kwa Hem na Skola) huendesha utafiti kati ya wazazi na watoto katika Elimu Msingi nchini Ufini. Uchunguzi hukusanya maelezo kuhusu jinsi wazazi wanafahamu na kupata elimu ya mtoto wao na ushirikiano kati ya nyumbani na shuleni. Wazazi hufikiria nini kuhusu masuala haya?
Uchunguzi wa wazazi, uliofanywa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Åbo, huwapa watunga sera, wafanyakazi wa shule, wazazi na washikadau wa shirika la wazazi maelezo muhimu kuhusu jinsi wazazi wanavyoiona shule ya watoto wao na ushirikiano na shule. Utafiti huo pia utasaidia Suomen Vanhempainliitto na Förbundet Hem och skola kupanga na kuendeleza shughuli zao. Pia ni muhimu kwamba shule ijifunze kuhusu jinsi wazazi wenye historia ya uhamiaji wanafahamu na kupata kusoma kwa watoto wao na ushirikiano na shule. Utafiti huo unatafasiriwa kwa lugha za kigeni zilizozungumzwa zaidi nchini Ufini
Maoni yako ni ya thamani! Tafadhali, jibu kidadisi kutoka kwa mtazamo wako. Ikiwa una watoto zaidi ya mmoja katika Elimu ya Msingi nchini Ufini, tafadhali jibu kidadisi ukifikiria kuhusu mmoja wao. Ikiwa unataka kujibu kwa mtoto zaidi ya moja, tafadhali jaza fomu tofauti ya kila mtoto. Kujibu kidadisi hiki ni kwa siri kabia na hakuna mhojiwa binafsi anayeweza kutambuliwa.
Utafiti huu umefunguliwa hadi Octoba 31, 2018. Inachukua dakika 30 kujibu kidadisi. Jibu maswali kwa kuashiria mbadala bora kwa maoni yako.
Hatimaye, kumbuka kutuma jibu lako kwa kubofya kitufe cha "Wasilisha".
Ikiwa unataka, unaweza kushiriki katika bahati nasibu ya vocha tatu yenye thamani ya yuro 100 kwa kujaza maelezo yako ya mawasiliano uliyotuma jibu. Jina lako halitaunganishwa kwenye kidadisi.
Maoni yako ni muhimu sana kwetu! Asante sana kwa kushiriki wako!
Ulla Siimes
Mkurugenzi Mkuu
Suomen Vanhempainliitto
gsm 040 553 0981
Micaela Romantschuk
Förbundet Hem och Skola
gsm 050 336 2016